CCM
Mlolongo wa Habari za Chama cha Mapinduzi

Tunataka mabadiliko Zanzibar
CHAMA cha Wananchi (CUF) kinaendesha kampeni ya kujenga imani kwa wananchi kwamba hakijapotea njia. Viongozi wake wa juu wanatembelea matawi wakieneza neno "Tuitambue Serikali ya Rais Karume."

Hoja ya Rais kushindwa kazi
- Serikali Kilosa ilivyopora wafugaji
NINACHANGIA mjadala ulioibuliwa na Profesa Ibrahim Lipumba, aliyesema Rais Jakaya Kikwete ameshindwa kazi; ukweli unaowakera wapambe wa Kikwete.

Nyerere kaondoka na CCM yake
MIAKA 10 baada ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuaga dunia, imedhihirika kuwa ameondoka na chama chake – Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Sakata la Posho mbili: Hakuna atakayepona
- Wapo waliochota hadi pensheni mbili kwa mkupuo
- Ni Kigoda, Ngwilizi, Mapuri na Mbatia
SAKATA la posho mbili kwa wabunge linatishia kumlipua hata Rais Jakaya Kikwete na viongozi kadhaa ndani ya Chama Cha Mapinduzi na serikali.

Digrii za Nchimbi, Kamala 'zaota mbawa'
- Sasa waamua kurejea darasani
- "Maprofesa" kibao nao wavuliwa wasifu
MAWAZIRI wawili wa serikali ya Rais Jakaya Kikwete, miongoni mwa sita waliotajwa kujipa wasifu wa elimu wasiyokuwa nayo, wameanza kutekeleza mkakati wa kujisafisha.

Mgawanyiko ndani ya CCM: Rais Kikwete anakimbia kivuli chake
UKWELI ni upi? Baadhi ya viongozi wa ngazi ya juu katika Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanakiri kuna mgawanyiko ndani ya chama chao.

Kikwete ameshindwa, ameangusha umma
NIMEVUTIWA na mjadala unaoendelea juu ya utendaji kazi wa Rais Jakaya Kikwete. Niseme kuwa Tanzania haijawahi kupata rais mwenye kutatanisha na aliyekatisha tamaa kama huyu wa sasa.

Chenge: Jasiri asiyeacha asili
JASIRI haachi asili! Ni Andrew Chenge. Wiki iliyopita, bila kutafuna maneno Chenge alithibitisha kuwa bado ni shujaa wa mikataba.

Wanaotaka kumuua Nyerere hawatafanikiwa
- Fikra zake zingali na thamani kwa taifa
- Nafsi yake bado imebeba tunu adimu
MWALIMU Julius Kambarage Nyerere, bado yu hai. Hili nililisema 14 Oktoba 1999, mara baada ya Rais Benjamin Mkapa kutangazia ulimwengu kuwa Mwalimu Nyerere amefariki dunia.

Mbinu za Magogoni zinavyojaribiwa majimboni
MALUMBANO kwa wadau wa uchaguzi Zanzibar yamefikia hatua mbaya.
Vyama vya upinzani hasa Chama cha Wananchi (CUF) vinaamini watu wapatao 170,000 hawatagusa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) na hivyo hawatapiga kura; matokeo yake itakuwa manufaa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho kwa Zanzibar, kinatajwa kupoteza kila uchaguzi tangu 1995.

Hatujafanikiwa kujisimamia
TUNAPOTAFAKARI hali ilivyokuwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika 25 Oktoba nchini kote, tunabaki kujiuliza, "Hivi kweli itafika siku tujivune mbele za watu kuwa tumefanikiwa kujisimamia?"

Mkakati wasukwa kumwangusha Spika Sitta
BAADA ya kukwama kwa jaribio la kwanza la kumng'oa Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta mjini Dodoma kupitia chama chake, sasa la pili linadaiwa kuandaliwa kwa ustadi.

Marando: Upinzani tumeaibisha
- Tumekipa upenyo Chama Cha Mapinduzi
MABERE Marando, mmoja wa waasisi wa mageuzi ya vyama vingi nchini, amesema ni aibu kwa vyama vya upinzani kushindwa kusimamisha wagombea katika sehemu nyingi nchini katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika Jumapili iliyopita.

Mfumo dume wa uchaguzi unadumaza demokrasia
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Celina Kombani anatamba: "Uchaguzi umefanikiwa kwa asilimia 98."

Hamza baba, uungwana unalipa
NAFURAHI kuona Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Kiongozi, Hamza Hassan Juma ameramba matapishi yake mwenyewe. Amegeuka.

Makamba ana ajenda gani?
YUSUPH Makamba, katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ana ajenda gani dhidi ya Spika wa Bunge la Jamhuri, Samwel Sitta?

Mressa kumvaa Mhita Kondoa Kaskazini
FRANK Mumba Mressa (30) ni miongoni mwa wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliojiingiza katika harakati za kuwania ubunge jimbo la Kondoa Kaskazini, mkoani Dodoma katika uchaguzi mkuu wa mwaka kesho.

Natamani fainali za CCM 2010
NATAMANI mwaka 2010 ufike haraka ili nione mshindi kati ya makundi mawili “hasimu” ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kikwete asaidie iwepo sera dhidi ya ufisadi
RAIS Kikwete Jumatano 09 Septemba, 2009, aliamsha hisia za wananchi kwa kutoa staili mpya ya kuwaruhusu kumweka kiti moto 'live' kwenye luninga na vituo vya redio hapa nchini.

Tunahitaji kinga ya kuvuana uanachama
KATIBA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) fungu la (1) Ibara ya 8(2) inatoa masharti ya mwanachama kwamba awe ni mtu anayefanya "juhudi ya kuelewa, kuieleza na kuitekeleza itikadi na siasa ya CCM."

Hoja ya mbunge Nyalandu bomu
- Imejaa chembechembe za udikiteta
HOJA binafsi ambayo mbunge Lazaro Samuel Nyalandu anataka kuwasilisha bungeni kuziba mijadala inayohusu imani na madhehebu – dini, haina maana.

CCM sasa chama cha kisultani - Shibuda
“NDANI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuna viongozi wanaoilewa vema misingi na maadili ya chama, lakini wapo wanachama wasiojua chochote kuhusu chama chao. Ni wale waliovunwa kwa njia ya ufisadi na uanachama wa papo kwa papo. Hawa ndio wanaokivuruga chama chetu.

Nini matarajio ya Jumamosi Pemba?
SIKU 38 baada ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kusitisha uandikishaji kwa ajili ya Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) la Zanzibar, kazi hiyo inaanza tena Jumamosi 12 Septemba 2009.

Acha Spika afanye kazi
TANZANIA haihitaji watu wakamilifu, kwani hawapo duniani; haihitaji watu watakatifu, kwa kuwa hawako mbinguni; taifa hili halihitaji watu wasiokosea, hao nao hawapatikani; bali taifa linahitaji watu ambao wanajua mapungufu yao.

Maji Marefu sasa ataka ubunge
NI saa tatu asubuhi ya 13 Agosti 2009, ninakutana na Steven Ngonyani, maarufu kama Profesa Majimarefu. Ni nje ya Hoteli ya Sunrise, mjini Korogwe, mkoani Tanga. Yupo kwenye harakati za kuhamasisha watu washiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, akiwa kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Vitambulisho vimeanza kutafuna wakubwa
ZOGO la kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, sasa siyo tena mgogoro kati ya serikali na Chama cha Wananchi (CUF) pekee. Ni zogo lililotapakaa hadi katika taasisi za serikali.

Bahi wazomea waziri, wataka uhakika
KILA panapogunduliwa madini nchini na makampuni ya nje kuanza kuchimba, mara moja maisha ya wananchi hubadilika kutoka kuwa ya bahati na kuwa ya balaa.

Anguko la CCM dhahiri
SERIKALI ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imekasirika. Sasa inashusha hasira zake kwa wabunge, Spika na Bunge lenyewe. Viongozi wanajua fika kuwa Bunge, kama Serikali na Mahakama, ni mhimili wa dola.

Maamuzi ya CCM Dodoma: Wananchi wahitaji chama mbadala
KABLA ya mikutano ya Dodoma ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wiki mbili zilizopita, ilikuwa rahisi kwa makada wa chama hicho kujinoma, kujitetea na angalau kudai wako mbali na zimwi la ufisadi.

CCM itamke ufisadi sera yake
UNAHITAJI kichwa kilichotulia kuchambua kwa mapana yaliyojiri kwenye vikao vya Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) vya Chama Cha Mapinduzi (CCM).