CHADEMA
Mlolongo wa Habari za Chama cha Demokrasia na Maendeleo

Kilichozimwa bungeni hiki hapa
SPIKA wa Bunge, Anna Makinda, mnamo 17 Julai, aliamuru sehemu ya hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusu makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani isisomwe kwa maelezo kwamba mambo yaliyomo yanaingilia uhuru wa mahakama.

JK abanwa mbavu
RAIS Jakaya Kikwete amepelekewa ujumbe kwamba bajeti ya serikali yake “ni ya madeni matupu, ahadi hewa na haitekelezeki,” MwanaHALISI linaweza kuripoti.

CCM inanengua midundo ya CHADEMA
NAFURAHISHWA na siasa za Tanzania sasa kwa maana moja kubwa, kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM), mbali ya kujigamba kuwa hakuna kiongozi wa chama vya upinzani ambaye hakutokana nacho, kwa vitendo, kimethibitisha kuwa sasa kinafundishwa siasa na vyama vya upinzani.

Makani atakumbukwa kwa ujasiri
MWASISI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bob Muhammad Nyanga Makani amefariki dunia na anatarajiwa kuzikwa leo nyumbani kwao Shinyanga.

Kimbunga CHADEMA chagusa mfupa wa CCM
MOJA ya agenda kubwa katika vikao vya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mjini Dodoma ilikuwa kuhusu ughali wa bei za vyakula na ugumu wa maisha unaowakabili Watanzania.

Dua la kuku la CCM laishindwa CHADEMA
KATIKA mchezo wa soka kuna mambo mengi yanayovutia mashabiki. Pale ligi inapokaribia mwisho, utasikia mengi zaidi, hasa kutokana na nafasi ya kila timu kunyakua ubingwa.

CHADEMA kufuta kinga ya Mkapa
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimebainisha maeneo matano ya kipaumbele katika “kipindi kifupi kijacho,” ili kujiimarisha miongoni mwa umma.

CCM, CHADEMA wanacheza zero distance
KUNA vita ya kugombania nchi ambayo inaendelea. Labda niseme vizuri zaidi kuwa kuna mpambano unaendelea wa kugombania nani atawale nchini; na katika hili hakuna urafiki, udugu, mapatano au umoja wa ulaghai.

Anguko kuu la CCM
USHINDI wa CHADEMA katika jimbo la Arumeru Mashariki, “ni ushahidi kwamba wananchi wakielewa watafanya mapinduzi ya kisasa.”

Mbatia: Tumefungua ukurasa mpya
SASA uwezekano wa vyama vya upinzani kuungana, kukabiliana na Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeanza kuonekana.

CHADEMA yamtega tena JK
RAIS Jakaya Kikwete aweza kukitosa tena Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuhusu uundwaji wa katiba mpya, MwanaHALISI limeelezwa.

Regia alifanya mengi makubwa
REGIA Estelatus Mtema hatunaye; ametutoka ghafla na kuacha majonzi. Ajali mbaya aliyopata saa 5.30 hivi Jumamosi iliyopita eneo la Ruvu mkoani Pwani ndiyo imepora maisha yake. Anatarajiwa kuzikwa kwao Ifakara, Kilombero.
Wazazi wanalia, ndugu na jamaa wanalia; waliokua, kusoma, kufanya kazi naye wanasikitika. Wanasiasa hasa wanachama, wafuasi na viongozi wa chama chake – Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wanaombeleza kumpoteza mbunge huyo kijana na mpambanaji.

Opulukwa: Nipo vitani Meatu, nitashinda
MBUNGE wa jimbo la Meatu, Meshack Opulukwa anapiga mayowe. Kwa miezi miwili hakuna anayemsikiliza. Amekuwa akihangaika kutafuta ufumbuzi baada ya serikali ya mkoa kuamuru operesheni ya kuhamisha kwa nguvu makazi ya watu katika kijiji cha Mwangudo, ndani ya jimbo analoliwakilisha.
Uhamishaji huo umefanywa kwa sababu ya kinachoelezwa wananchi “wanaishi ndani ya hifadhi ya jamii ya Makao.” Matokeo ya operesheni hiyo ni kuteketezwa kwa moto zaidi ya nyumba 1,000 za wananchi na mamia ya watu kuumia.

Kikwete akaliwa kooni
- Naye atakiwa kujiuzulu
- Waraka mzito wavuja
- CHADEMA yaitwa ‘mchawi’
RAIS Jakaya Kikwete amekaliwa kooni. Wakati chama chake kinakabiliwa na wimbi la kukimbiwa na wanachama na viongozi, swahiba wake anashikilia kuwa wenye “tuhuma za ufisadi” wajiuzulu kama yeye.

Waziri kumkimbia Lowassa CCM
WAZIRI mmoja mwandamizi ndani ya serikali ya Rais Jakaya Kikwete, yuko mbioni kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM), imefahamika.

CHADEMA yatikisa Ikulu
RAIS Jakaya Kikwete hakufahamu kwa undani kilichomo kwenye muswada wa sheria ya mabadiliko ya katiba (Constitutional Review Bill 2011), uliopitishwa na bunge hivi karibuni, MwanaHALISI limeelezwa.

CCM: Kutema tamu, kumeza chungu
KAMPENI za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga, mkoani Tabora zinatarajiwa kuanza mjini humo Alhamisi wiki hii. Tayari viroja vya wanasiasa vimeanza na anayetegemea kuona au kusikia matumizi ya akili huko Igunga anajisumbua. Huu utakuwa mwezi wa kupumzisha akili na ukweli, kisha kutumia unafiki na uwongo ili kunogesha siasa za nchi yetu.
Kwa hali ilivyo ni mchuano kati ya CHADEMA na vyama vingine.

CHADEMA wametoa somo, lizingatiwe
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewafuta uanachama madiwani wake watano wa mkoa wa Arusha. Wengine wanasema haya ndiyo maamuzi magumu.

Mchungaji Msigwa: Tuna viongozi legelege
HANA makeke. Ni mpole, lakini mwenye msimamo thabiti wa kutetea anachokiamini. Si mwingine, bali Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Bunge la Muungano katika jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Taa ya njano yaiwakia CHADEMA
RANGI ya njano imetumika mahali pengi kama alama ya tahadhari. Wanaoendesha vyombo vya moto kama vile magari na pikipiki wanajua kwamba taa ya njano ikiwaka inamtahadharisha dereva kujiandaa kuchukua uamuzi; kusimama au kuendelea kuendesha.

CCM karibu ife: Vijana wafuate nini huko?
GAZETI la Citizen la 20 Aprili 2011, lilichapisha makala ya Ayub Rioba, ikimsifu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilson Mukama, kwamba ni mtu mwenye uwezo wa kukifufua chama hicho.

Unafiki wa CHADEMA, ulafi wa CCM
TAKRIBANI majuma mawili sasa, Bunge la Jamhuri na baadhi ya vyombo vya habari nchini vimetawaliwa na mjadala wa posho za wabunge na watumishi wa serikali.

Spika Makinda, kazi kwako!
FEBRUARI 6, 2008, Spika wa Bunge la 9 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliyekuwa Spika wa Bunge, Samweli Sitta alitoa dokezo zito kuhusu naibu wake Anne Makinda.

Mbunge: Katiba imevunjwa
HOJA ya Rais Jakaya Kikwete kusaini Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011-2016) kabla bunge kuujadili, imeibua shutuma kwa ofisi kuu nchini.

CCM wapanga kuhujumu CHADEMA
MKAKATI wa makusudi umesukwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kudhoofisha jitihada za kisiasa za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), MwanaHALISI limeelezwa.

Ukombozi waja… kipigo chayoyoma
NJIA bora ya kuharakisha mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi nchini Tanzania ni kubughudhi viongozi wa upinzani kila kukicha.

Matatizo mengine CHADEMA mnajitakia
UCHAGUZI mkuu wa kuchagua viongozi wa Baraza la Vijana la CHADEMA (BAVICHA) umekuja na mambo yake. Mengine yalitarajiwa na mengine hayakutarajiwa.

NEC na uparaganyaji siasa KigomaUjiji
JIMBO la Uchaguzi la Kigoma Mjini limekuwa na upinzani mkubwa kisiasa unaohusisha vyama vya CCM na CHADEMA kwa kipindi chote tangu mfumo wa vyama vingi uliporudishwa mwaka 1992.

Maandamano haya yaungwe mkono
NIMEFUATILIA kwa muda maandamano yanayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) toka mwanzo wake na nimejaribu kutumia muda kuyaelewa. Mwanzoni niliyaona kama maandamano ya watu ambao bado wana machungu ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa 30 Oktoba 2010.

Benson: CCM incheza ngoma ya CHADEMA
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakikushinda uchaguzi mkuu mwaka 2010 kiliangushwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).