Dowans
Mlolongo wa Habari za kashfa ya Dowans

Wakiwalipa Dowans, tuwalipishe
NINAZO habari mbili; moja mbaya nyingine nzuri. Kwanza, ni mkataba ambao Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) ilifunga na kampuni ya Richmond na kujiweka chini ya usuluhishi wa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi (ICC) bila ya kuwa na nafasi ya kukataa rufaa.

Kikwete utachomoka Dowans?
NIMESOMA maandiko ya baadhi ya waandishi waliohoji, nani aliyetufikisha hapa katika sakata hili la Dowans?

Rostam ndiye Dowans
MJUMBE wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ni moja ya nguzo kuu ndani ya kampuni ya kufua umeme ya Dowans, imefahamika.

Salva ikulu imebaki uchi
SALVATORY Rweyemamu, aliyekuwa mkurugenzi na mhariri mtendaji wa Habari Corporation Ltd (HCL), ni mtu wa kuhurumiwa sana. Amepata kazi ngumu.

Dowans inatusukuma kudai katiba mpya
WATANZANIA wanatakiwa kulipa Sh. 94 bilioni ambazo Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) imeitunuku kampuni ya Dowans kwa mkataba wake na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kukatishwa.

Dowans wakubuhu wizi
VIGOGO ndani ya serikali wanatuhumiwa kupanga njama za kutaka kuilipa inyemela mabilioni ya shilingi kampuni ya Dowans, kabla taratibu muhimu kuhitimishwa.

Dowans ni chuma ulete wa ikulu?
HERI ya Mwaka Mpya wapenzi wasomaji wa safu hii ya Wazo Mbadala inatolewa wakati bei mpya ya umeme imeanza.

Rais Kikwete ajinasue Dowans
SERIKALI ya Rais Jakaya Kikwete imejipambanua sasa kuwa ina ubia au inafadhili miradi ya kifisadi, ukiwemo huu wa kutaka kuichotea kampuni feki ya Dowans Sh. 185 milioni ambazo ni kodi ya wananchi.

Wamiliki wa Dowans wanafahamika
KWA MUDA mrefu sasa, jamii na vyombo vya habari vimekuwa vinashinikiza serikali imtaje mmiliki au wamilki wa kampuni ya Dowans ambayo ilishinda kesi hivi karibuni dhidi ya serikali na kuamriwa ilipwe Sh. Bilioni 185.

Ya Dowans ni kashfa nyingine serikalini
HAKUNA ubishi kwamba uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Biashara (ICC), unaotaka serikali kulipa Dowans fidia ya Sh.185 bilioni, ni hujuma kwa taifa na kashfa nyingine ndani ya kashfa.

Wezi wa Dowans hawa
MAFISADI watatu waliojipanga kuchota Sh. 185 bilioni kutoka serikalini, zikiwa fidia kwa kuvunja mkataba wa kampuni ya kufua umeme ya Dowans, wamefahamika.

Nani anayekabidhiwa fedha ya Dowans?
WAZIRI Mkuu wa Jamhuri, Mizengo Pinda amejitwisha zigo lisilobebeka. Litamuangusha. Ameahidi kulipa mabilioni ya shilingi kwa kampuni ya kufua umeme wa dharula, Dowans Holding Tanzania Limited.

Dowans kuifilisi Tanesco
SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco) liko hoi kiuchumi na halikopesheki, MwanaHALISI imeelezwa.

Dowans: Matokeo ya serikali ya kifisadi
KILA ninapotafakari masuala mbalimbali, huishia kujiuliza, Je, katika mapambano yoyote yanayofanywa na binadamu (ya vita, ya siasa au mengineyo), Mwenyezi Mungu huwa anakaa upande gani – wa wanyonge au upande wa wababe?

FIDIA DOWANS: Wizi uleule, wezi walewale katika suti mpya
WATUHUMIWA wakuu wa ufisadi nchini wanashangilia. Waliojiita wapambanaji, wanazomewa. Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO), linajikuta lipo katikati na sasa linalazimika kutii agizo la mahakama.

'Tunaogopa Dowans kama baba mkwe'
NI hatari sana kuwa na viongozi woga. Ni hatari zaidi kuwa na viongozi wasio na maono. Ni hatari iliyopita kiasi kuwa na viongozi wasio wakweli kwa wanaowaongoza.

Serikali inaihujumu TANESCO kwa ajili ya Dowans?
KWA mara nyingine, serikali, kupitia Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO), imetangaza mgawo wa umeme ambao utaathiri mikoa yote inayopata umeme kupitia gridi ya taifa.

Kikwete ametuacha njia panda
HOTUBA ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa 1 Aprili 2009, haiwezi kupita bila kujadiliwa. Sababu zipo nyingi. Lakini kubwa ni kwamba hotuba ya rais ni kichocheo cha mijadala.

Lipumba aulizwe alipojikwaa
MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi (CUF) Profesa Ibrahim Lipumba, amejitosa katika sakata la ununuzi wa mitambo ya Dowans.

Mafisadi wamtishia Kikwete
WATUHUMIWA wa ufisadi, wanaolalamika kuwa Rais Jakaya Kikwete amewatelekeza, wanapanga kumhusisha katika baadhi ya tuhuma zinazowakabili ili kumshinikiza kutimiza matakwa yao, MwanaHALISI limeelezwa.

Mwakyembe: Nitafyatuka
- Lissu: Dharura ni kichaka cha ufisadi
MBUNGE wa Kyela (CCM), Dk. Harisson Mwakyembe amembwatukia mfanyabiashara Rostam Aziz na kumwonya kuwa “kuna siku tutafyatuka…tusiheshimiane kabisa.”

Mwakyembe akoromea Rostam
JUMATANO iliyopita mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe alikutana na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, kujibu kile alichoita, “kombora” alilotupiwa. Ifuatayo ni sehemu iliyofupishwa ya maelezo yake, ikifuatiwa na mahojiano kati yake na waandishi.

Ngeleja sasa amwacha Zitto ulingoni
- SAKATA LA DOWANS
HITIMISHO la mjadala wa ununuzi wa mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans Holding (Tanzania) Limited, bado halijafikiwa.

Zitto amejikwaa, hajaanguka
MSIMAMO wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuhusu suala la ununuzi wa mitambo ya kuzalisha umeme ya Dowans unaonekana kuwakwaza watu wengi.

Sakata la Dowans: Waziri Ngeleja siyo mkweli
SAKATA la ununuzi wa mitambo ya kufua umeme kutoka kampuni ya Dowans Holding (Tanzania) Limited, halijapatiwa ufumbuzi.

Dk. Rashid, TANESCO na Dowans: Ndoa iliyoshindikana alfajiri
KWA mara nyingine, serikali kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO) imetangaza kujitoa katika mipango ya kununua mitambo ya kampuni ya Dowans Holding (Tanzania) Limited.

Rostam kinara wa Dowans
- Anajuana na Dowans, Kagoda
- Serikali yamwangalia tu
MWANASIASA na mfanyabiashara Rostam Aziz ana siri kubwa kuhusu makampuni ya Dowans na Kagoda Agriculture Limited yanayotuhumiwa kwa kuhujumu uchumi.

Dowans ina harufu ya Lowassa
TAREHE 7 Februari 2008 aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa alilazimika kuachia ngazi nafasi hiyo kutokana na kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond Development Company (LLC).

Sakata la Dowans: Serikali kuchafuka upya
KELELE za sasa ndani ya serikali kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans ni jitihada zinazolenga “kukidhi maslahi binafsi,” MwanaHALISI limegundua.

Bunge likatae kubeba serikali
KATIKA hali ya kawaida, haitegemewi serikali kutumia bunge kutekeleza mambo yake; wala haitarajiwi bunge kufanya kazi zake kwa kuitumia serikali.